Chapter 96 (Sura 96)
1; Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
2; Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
3; Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
4; Ambaye amefundisha kwa kalamu.
5; Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
6; Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
7; Akijiona katajirika.
8; Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
9; Umemwona yule anaye mkataza
10; Mja anapo sali?
11; Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
12; Au anaamrisha uchamngu?
13; Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
14; Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
15; Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
16; Shungi la uwongo, lenye makosa!
17; Basi na awaite wenzake!
18; Nasi tutawaita Mazabania!
19; Hasha! Usimt´ii! Nawe sujudu na ujongee!
Swahili Quran | Soma Kurani
Pages: 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 84 85 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 108 109 110 111 112 113 114