Chapter 88 (Sura 88)
1; Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
2; Siku hiyo nyuso zitainama,
3; Zikifanya kazi, nazo taabani.
4; Ziingie katika Moto unao waka –
5; Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
6; Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
7; Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
8; Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
9; Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
10; Katika Bustani ya juu.
11; Hawatasikia humo upuuzi.
12; Humo imo chemchem inayo miminika.
13; Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
14; Na bilauri zilizo pangwa,
15; Na matakia safu safu,
16; Na mazulia yaliyo tandikwa.
17; Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
18; Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
19; Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
20; Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
21; Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
22; Wewe si mwenye kuwatawalia.
23; Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
24; Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
25; Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
26; Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
Swahili Quran | Soma Kurani
Pages: 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 84 85 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 108 109 110 111 112 113 114