Chapter 91 (Sura 91)
1; Naapa kwa jua na mwangaza wake!
2; Na kwa mwezi unapo lifuatia!
3; Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
4; Na kwa usiku unapo lifunika!
5; Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
6; Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
7; Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
8; Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
9; Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
10; Na hakika amekhasiri aliye iviza.
11; Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
12; Alipo simama mwovu wao mkubwa,
13; Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
14; Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
15; Wala Yeye haogopi matokeo yake.
Swahili Quran | Soma Kurani
Pages: 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 84 85 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 108 109 110 111 112 113 114