Chapter 81 (Sura 81)
1; Jua litakapo kunjwa,
2; Na nyota zikazimwa,
3; Na milima ikaondolewa,
4; Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
5; Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
6; Na bahari zikawaka moto,
7; Na nafsi zikaunganishwa,
8; Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
9; Kwa kosa gani aliuliwa?
10; Na madaftari yatakapo enezwa,
11; Na mbingu itapo tanduliwa,
12; Na Jahannamu itapo chochewa,
13; Na Pepo ikasogezwa,
14; Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
15; Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
16; Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
17; Na kwa usiku unapo pungua,
18; Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
19; Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
20; Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
21; Anaye t´iiwa, tena muaminifu.
22; Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
23; Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
24; Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
25; Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
26; Basi mnakwenda wapi?
27; Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
28; Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
29; Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Swahili Quran | Soma Kurani
Pages: 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 84 85 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 108 109 110 111 112 113 114