Chapter 89 (Sura 89)
1; Naapa kwa alfajiri,
2; Na kwa masiku kumi,
3; Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
4; Na kwa usiku unapo pita,
5; Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
6; Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A´di?
7; Wa Iram, wenye majumba marefu?
8; Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
9; Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
10; Na Firauni mwenye vigingi?
11; Ambao walifanya jeuri katika nchi?
12; Wakakithirisha humo ufisadi?
13; Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
14; Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
15; Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
16; Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
17; Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
18; Wala hamhimizani kulisha masikini;
19; Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
20; Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
21; Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
22; Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
23; Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
24; Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
25; Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
26; Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
27; Ewe nafsi iliyo tua!
28; Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
29; Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
30; Na ingia katika Pepo yangu.
Swahili Quran | Soma Kurani
Pages: 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 84 85 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 108 109 110 111 112 113 114