Chapter 92 (Sura 92)
1; Naapa kwa usiku unapo funika!
2; Na mchana unapo dhihiri!
3; Na kwa Aliye umba dume na jike!
4; Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
5; Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
6; Na akaliwafiki lilio jema,
7; Tutamsahilishia yawe mepesi.
8; Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
9; Na akakanusha lilio jema,
10; Tutamsahilishia yawe mazito!
11; Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
12; Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
13; Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
14; Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
15; Hatauingia ila mwovu kabisa!
16; Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
17; Na mchamngu ataepushwa nao,
18; Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
19; Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
20; Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
21; Naye atakuja ridhika!
Swahili Quran | Soma Kurani
Pages: 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 84 85 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 108 109 110 111 112 113 114