Chapter 85 (Sura 85)
1; Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
2; Na kwa siku iliyo ahidiwa!
3; Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
4; Wameangamizwa watu wa makhandaki
5; Yenye moto wenye kuni nyingi,
6; Walipo kuwa wamekaa hapo,
7; Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
8; Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
9; Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
10; Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
11; Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
12; Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
13; Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
14; Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
15; Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
16; Atendaye ayatakayo.
17; Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
18; Ya Firauni na Thamudi?
19; Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
20; Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
21; Bali hii ni Qur´ani tukufu
22; Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.
Swahili Quran | Soma Kurani
Pages: 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 84 85 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 108 109 110 111 112 113 114