Chapter 100 (Sura 100)
1; Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
2; Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
3; Wakishambulia wakati wa asubuhi,
4; Huku wakitimua vumbi,
5; Na wakijitoma kati ya kundi,
6; Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
7; Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
8; Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
9; Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
10; Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
11; Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
Pages: 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 84 85 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 108 109 110 111 112 113 114